DIEGO JOTA AFARIKI DUNIA KWA AJARI YA GARI.


 Mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Ureno, Diogo Jota, ameripotiwa kufariki dunia katika ajali mbaya ya gari iliyotokea nchini Hispania, karibu na eneo la Zamora, kaskazini magharibi mwa nchi hiyo na kwa mujibu wa shirika la habari la EFE la Hispania, ajali hiyo ilitokea siku ya Jumanne na imethibitishwa na vyanzo kadhaa vya karibu na familia.

Jota, mwenye umri wa miaka 28, alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa Liverpool tangu alipojiunga na klabu hiyo mwaka 2020 akitokea Wolverhampton Wanderers kwa ada ya zaidi ya pauni milioni 40 vile vile alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na kasi, uwezo wa kufunga na nidhamu uwanjani na kabla ya tukio hili la kusikitisha Jota alikuwa ameoa wiki chache zilizopita na alikuwa na familia ndogo yenye furaha pamoja na watoto wake watatu.

Habari za kifo chake zimepokewa kwa mshtuko mkubwa na mashabiki wa soka duniani kote huku wengi wakituma salamu za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii na klabu ya Liverpool, mashabiki wake pamoja na jamii ya soka kwa ujumla wanakumbuka mchango mkubwa wa Jota katika mchezo huo na kuomboleza kuondokewa na mchezaji aliyeacha alama isiyofutika.

Comments